Mfumo wa kielektroniki wa huduma za afya nchini Tanzania, unaojulikana kama GoTHOMIS (Government of Tanzania Health Operations Management Information System), ni mfumo ambao umeundwa na serikali ya Tanzania ili kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa wananchi. GoTHOMIS ni jukwaa ambalo linasaidia katika usimamizi wa taarifa za afya, kurahisisha mawasiliano ya huduma za afya, na kutoa takwimu muhimu kwa wachambuzi na watunga sera. Mfumo huu una umuhimu mkubwa kwani unarahisisha mipango na usimamizi wa rasilimali za afya, kuimarisha utoaji wa huduma, na kuboresha ufanisi na ubora wa huduma kwa wananchi.
Jinsi ya Kujiunga au kujisajili na Mfumo wa GoTHOMIS
Kujiunga na mfumo wa GoTHOMIS unahitaji kufuata hatua kadhaa ili kuhakikisha taarifa na huduma zako za afya zinaweza kufikiwa kwa urahisi.
- Kwanza, unahitaji kuwasiliana na wataalamu wa Tehama wa halmashauri au kituo husika ili kupatiwa maelekezo zaidi juu ya jinsi ya kujiunga. Wataalamu hawa wanapatikana kwenye vituo vya afya vilivyopo kwa usajili wa huduma za GoTHOMIS.
- Pia, unaweza kuwasiliana na mganga mfawidhi wa kituo chako ili kuhakikisha kama kituo chako kimeanza kutumia mfumo wa GoTHOMIS. Kwa maswala ya kiufundi au msaada zaidi, unaweza kuwasiliana na timu yako ya ICT Support ili kupata maelekezo na mwongozo wa namna ya kujiunga na mfumo huu muhimu.
Jinsi ya kuingia kwenye akaunti yako ya GoTHOMIS
Mara baada ya kujiunga na mfumo wa GoTHOMIS, kuingia kwenye akaunti yako ni rahisi.

- Kwanza, fungua tovuti rasmi ya GoTHOMIS, ambapo utapata sehemu ya ‘Sign In’ au ingia kupitia linki hii hapa : www.gothomis.tamisemi.go.tz/. Hapa utahitajika kuingiza ‘Username’ yako na ‘Password’ uliyopewa wakati wa usajili.
- Kama umesahau neno lako la siri, usihangaike! Unaweza kubofya sehemu iliyoandikwa ‘Forgot Password’ ili kupata maelekezo ya jinsi ya kurudisha neno la siri lako.
- Hakikisha unajaza taarifa zako sahihi ili kuingia kwenye akaunti yako kwa urahisi. Mara baada ya kuingiza taarifa zako, bofya kitufe cha ‘Sign In’ ili kufungua akaunti yako na kufikia huduma mbalimbali zinazotolewa katika mfumo wa GoTHOMIS.
Sehemu au Vipengele muhimu vya Mfumo wa GoTHOMIS
Mfumo wa GoTHOMIS unajumuisha vipengele muhimu ambavyo vitakusaidia kupokea na kusimamia huduma za afya kwa ufanisi. Baadhi ya vipengele hivi ni:
- TB and Leprosy Information and Management – Inatoa njia za kusimamia taarifa na huduma za ugonjwa wa kifua kikuu na ukoma.
- Neonatal Intensive Care Unit (NICU) – Kituo cha Huduma ya Watoto Walioko kwenye Hali Mbadala, ambacho kinatoa huduma za uangalizi maalum kwa watoto wachanga.
- Outpatient Consultation – Huduma za wagonjwa wa nje zinazoangazia historia ya mgonjwa, majadiliano, uchunguzi, na matibabu.
- Patient Registration – Usajili wa wagonjwa ambapo unaweza kufanya usajili, kuhakiki kadi, na kuweka miadi.
- Pharmacy Management – Usimamizi wa dawa ukiwa na huduma za maombi, upokeaji, utoaji, na kupokea dawa.
- Vital Signs – Huduma za kuchunguza viashiria vya afya kama vile ishara muhimu na BMI.
- Prime Vendor – Huduma za utoaji taarifa za OOS (Out of Stock), maagizo, na usimamizi wa fedha.
- Diabetes and Hypertension – Huduma za usajili, ushauri na kuratibu miadi ya wagonjwa wenye kisukari na shinikizo la damu.
- Bill Management – Usimamizi wa bili ambapo unaweza kuona bili zinazokaribia kulipwa, zilizofutwa, na kurudia stakabadhi.
- Nursing Care – Huduma maalum za uuguzi ikiwemo ombi la kulazwa, orodha ya wagonjwa walioruhusiwa, na kadi za kumbukumbu.
- Operating Theater – Sehemu ya kupata idhini za upasuaji, hali kabla ya operesheni, na ziara za daktari wa ganzi.
- Inpatient Consultation – Huduma za ushauri kwa wagonjwa wa ndani, ikihusisha historia ya mgonjwa na matibabu.
- External Referral – Huduma za rufaa za dharura na za kawaida, pamoja na kupokea kesi za marejeo.
- Insurance Management – Usimamizi wa bima unaohusisha uthibitisho wa bima na uwasilishaji wa madai ya kielektroniki.
- Insurance Management – Usimamizi wa bima ambapo huduma za uhakiki wa bima za NHIF, CHF, na uwasilishaji wa madai na idhini ya huduma unawezekana.
Kwa kutumia mfumo wa GoTHOMIS, utaweza kufikia huduma hizi zote kwa urahisi na kwa ufanisi zaidi. Mfumo huu unalenga kuboresha utoaji wa huduma za afya na kuhakikisha kuwa wananchi wanapata huduma bora zaidi.